H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I)...

15
Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HA AR RR RI IS SO ON N U UW WA AT TA A G GI IR RL LS S S SE EC CO ON ND DA AR RY Y S SC CH HO OO OL L Email: [email protected] Website: www.uwata.or.tz / www.harrisongirls.ac.tz EDUCATION IS A SUSTAINABLE ASSET______________________________________________________________________________ YAH: TAARIFA YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 Mzazi/Mlezi wa _________________________________ Ninafurahi kukutaarifu kuwa mwanao amechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule yetu. Hongera sana. Shule inamilikiwa na Uamsho wa Wakristo Tanzania ( UWATA) na inawapokea wanafunzi kutoka mazingira mbalimbali pamoja na dini zote. Tunawalea wanafunzi kwa misingi ya kumhofu na kumtanguliza Mungu kwa kila jambo, tunasisitiza nidhamu pamoja na kutoa Elimu bora itakayomwezesha mwanafunzi kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha katika ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia.Hivyo uchaguzi wako wa kumleta mwanao Harrison Uwata ni sahihi. KARIBU SANA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA HARRISON UWATA “Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee” (Mithali 22:5) Shule ni ya BWENI, hivyo utalazimika kugharimia gharama zote za mwanafunzi wa Bweni kwa kufuata mchanganuo uliofafanuliwa katika fomu ya kujiunga na shule iliyoambatanishwa na barua hii. Hata hivyo utatakiwa kujaza fomu zifuatazo na kuzirudisha siku ya kuwasili shuleni. 1. Fomu ya uchunguzi wa Afya (Medical Examination Form) 2. Fomu ya taarifa binafsi za mwanafunzi. 3. Tamko rasmi la kukubali kujiunga na shule 4. Fomu ya utii wa sheria, kanuni za shule na Tabia njema. Shule ipo jijini Mbeya eneo la Iwambi Mita50 kutoka barabara kuu iendayo Zambia upande wa kusini mwa barabara. ● Wanafunzi wanaotokea mikoa ya kanda ya ziwa, kanda ya kati kanda ya kaskazini,kanda ya magharibi, kanda ya mashariki na mikoa ya Iringa,Njombe na Ruvuma wakifika stendi ya Nane nane au stendi kuu ya Mbeya wapande daladala zinazokwenda Mbalizi na washuke kituo cha Iwambi. Lakini pia wanafunzi wanaotokea mkoa wa Dar es salaam waweza kupanda mabasi

Transcript of H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I)...

Page 1: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 1 kati ya 15

HHHAAARRRRRRIIISSSOOONNN UUUWWWAAATTTAAA GGGIIIRRRLLLSSS’’’ SSSEEECCCOOONNNDDDAAARRRYYY SSSCCCHHHOOOOOOLLL

Email: [email protected]

Website: www.uwata.or.tz /

www.harrisongirls.ac.tz

“EDUCATION IS A SUSTAINABLE ASSET”

______________________________________________________________________________

YAH: TAARIFA YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA

MWAKA 2020

Mzazi/Mlezi wa _________________________________

Ninafurahi kukutaarifu kuwa mwanao amechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika

shule yetu. Hongera sana.

Shule inamilikiwa na Uamsho wa Wakristo Tanzania (UWATA) na inawapokea wanafunzi

kutoka mazingira mbalimbali pamoja na dini zote. Tunawalea wanafunzi kwa misingi ya

kumhofu na kumtanguliza Mungu kwa kila jambo, tunasisitiza nidhamu pamoja na kutoa Elimu

bora itakayomwezesha mwanafunzi kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha katika

ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia.Hivyo uchaguzi wako wa kumleta mwanao Harrison

Uwata ni sahihi.

KARIBU SANA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA HARRISON UWATA

“Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee”

(Mithali 22:5)

Shule ni ya BWENI, hivyo utalazimika kugharimia gharama zote za mwanafunzi wa Bweni

kwa kufuata mchanganuo uliofafanuliwa katika fomu ya kujiunga na shule iliyoambatanishwa

na barua hii. Hata hivyo utatakiwa kujaza fomu zifuatazo na kuzirudisha siku ya kuwasili

shuleni.

1. Fomu ya uchunguzi wa Afya (Medical Examination Form)

2. Fomu ya taarifa binafsi za mwanafunzi.

3. Tamko rasmi la kukubali kujiunga na shule

4. Fomu ya utii wa sheria, kanuni za shule na Tabia njema.

Shule ipo jijini Mbeya eneo la Iwambi Mita50 kutoka barabara kuu iendayo Zambia upande

wa kusini mwa barabara.

● Wanafunzi wanaotokea mikoa ya kanda ya ziwa, kanda ya kati kanda ya

kaskazini,kanda ya magharibi, kanda ya mashariki na mikoa ya Iringa,Njombe na

Ruvuma wakifika stendi ya Nane nane au stendi kuu ya Mbeya wapande daladala

zinazokwenda Mbalizi na washuke kituo cha Iwambi.

Lakini pia wanafunzi wanaotokea mkoa wa Dar es salaam waweza kupanda mabasi

Page 2: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 2 kati ya 15

yaendayo Tunduma kisha washuke stand ya Iwambi.

● Wanafunzi wanaotokea Rukwa,Tunduma na Mbozi washuke kituo cha Iwambi

● Mwanafunzi akifika kituo cha Iwambi aweza kutembea kwa miguu kuelekea

mwelekeo wa bara bara iendayo Tunduma ambako baada ya mita chache mbele

ataona kibao cha HARRISON-UWATA upande wa kushoto kitakachomwelekeza

sehemu shule ilipo.

MUHIMU:

Mwanafunzi anatakiwa kuripoti shuleni siku ya Ijumaa tarehe 03/01/2020 bila kukosa.

Endapo atachelewa kuripoti kwa muda wa siku tatu kuanzia tarehe ya kufungua shule, nafasi

yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine.

SEHEMU A: MASOMO YANAYOFUNDISHWA KIDATO CHA KWANZA

Civics, History, Geography, Kiswahili, English Language, Basic

Mathematics, Chemistry, Physics, Biology, Computer & Bible knowledge.

SEHEMU B:

1. GHARAMA YA ADA KWA MWAKA 2020.

Karo pamoja na gharama za Hosteli ni Tsh 2,100,000/=

S/N KIASI MUDA WA KULIPA

1 300,000/= Lipa kabla ya 02 Novemba, 2019 kwa ajili ya kushika nafasi.

Kushindwa kufanya hivyo nafasi yako atapewa mtu mwingine.

2 450,000/= Lipa kabla ya 02 Januari 2020

3 400,000/= Lipa kabla ya 03 Aprili 2020

4 550,000/= Lipa kabla ya 02 Julai 2020 5 400,000/= Lipa kabla ya 03 Septemba 2020

JUMLA 2,100,000/= Ilipwe kupitia akaunti ya shule

2. GHARAMA ZA MAHITAJI MENGINE

Na. MAHITAJI KIWANGO MAELEZO

1 Sare za shule 200,000/= Atapewa,sketi mbili, shamba dress moja, shati mbili,

t-shirt moja, tai mbili, sweta moja, jezi na suruali

yake, sketi ya michezo, trucksuit, mzura na gloves (za

kuvaa wakati wa baridi).

2 Mazingira, afya

na uchakavu

130,000/=. Uboreshaji mazingira, uchakavu wa samani za shule

na huduma ya kwanza

JUMLA 330,000/= Ilipwe kupitia akaunti ya shule

Akaunti za shule :

i. CRDB a/c no; 01j1065414702 (UWATA EDUCATION CENTRE)

ii. NMB a/c no; 62206600077 (HARRISON UWATA GIRLS’ HIGH SCHOOL)

Page 3: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 3 kati ya 15

MICHANGO YA KITAALUMA NA MAHITAJI YA MWANAFUNZI MWAKA 2020

A: MICHANGO YA KITAALUMA

Na AINA YA MCHANGO KIASI

1 Mtihani wa pamoja wa Jiji, Ujirani mwema pamoja na

masomo ya ziada (Remedial)

Tsh. 50,000/=

2 Rimu mbili za A4 (Rimu moja kwa kila muhula).

B: MAHITAJI YA MWANAFUNZI

Na AINA YA MCHANGO KIASI

1 Kulipia godoro kwa mwaka mzima.

Tsh. 20,000/=

2 Vyombo vya chakula (Sahani na kikombe) Tsh. 5,000/=

3 Fedha ya matumizi binafsi ya mwanafunzi (Pocket Money)

pamoja na kunyoa nywele.

Tsh. 107,000/=

(Tsh. 53,500/= kwa muhula).

NB:

Fedha hizi zote ziletwe mkononi siku ya kuripoti shuleni.

Page 4: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 4 kati ya 15

Tafadhali zingatia haya:

o Kulipa ada na michango mingine kwa wakati uliopangwa

o Ifahamike kwamba taasisi ya UWATA ina akaunti nyingi, hivyo zingatia kulipia kwenye

akaunti husika hapo juu.

o Kumbuka kuandika jina la mwanafunzi kwenye Bank pay in slip (risiti ya benki)

unapolipa ada na michango kwenye akaunti na uje nayo shuleni siku ya kuripoti.

Mahitaji mengine ya mwanafunzi anayotakiwa kuja nayo au kununua kwenye duka la shule ni

kama ifuatavyo:

(i) Blanketi moja. 1pc, @ 15,000/= au Tsh 35,000/=

(ii) Taulo mbili. 1pc @ 8,000/=

(iii) Khanga doti 2 @ Tsh 8,000/= au kitenge doti 2 @ 17,000/=

(iv) Shuka 2 (Moja rangi ya pinki na moja ya bluu) @ 6,500/=

(v) Ndoo moja ya kuogea na kufulia 3,500/=

(vi) Kijiko Tsh. 500/=

(vii) Toilet papers za kutosha @ Tsh. 1,000/=

(viii) Chandarua Tsh. 8,500/=

(ix) Aje na Raba nyeusi za michezo.

(x) Aje na Picha ndogo 4 (Passport size)

(xi) Pia anatakiwa kuja na nguo binafsi (za nyumbani) zisizozidi jozi mbili na ya tatu

atakayokuwa amevaa siku anapowasili shuleni, ziwe ndefu na zisizoangaza. Nguo /

Blauzi iwe na mikono mirefu au ikiwa ni mikono mifupi iwe usawa wa kiwiko cha

mkono.

(xii) Viatu vyeusi vyenye kisigino kifupi na vyenye kamba, jozi 2 (visivyo na kamba

haviruhusiwi) pamoja na viatu vyeusi vya wazi vyenye mkanda nyuma vya kushindia

(Flat Open shoes) jozi moja tu na ndala za kuogea na sio yeboyebo. Simple shoes

haziruhusiwi. (xiii) Soksi nyeupe za kutosha zenye urefu wa kati. @ 1,000/= (Soksi za rangi nyingine

iwayo yoyote haziruhusiwi).

(xiv) Jaketi la aina yoyote hairuhusiwi, isipokuwa sweta la shule tu.

(xv) Daftari kumi na moja (11) za aina ya kaunta (4 QUIRE) @ 4,500/= pamoja na daftari

ndogo kumi na moja za mazoezi zenye kurasa 200. @ 1,500/=

(xvi) Begi la saizi ya kati la kuhifadhia vitu vyake na sio sanduku la bati(Trunker)

(xvii) Vibanio vya kuanikia nguo(jozi mbili) @ 2,000/=

(xviii) Aje na brash ngumu ya mkono ya kusugulia sinki na squeezer (skwiza) yakusugulia

sakafu.

(xix) Aje na File kubwa la kuwekea mitihani yake (Box file) tsh. 3,500/=, kalamu za wino

(pens) zisizopungua kumi @ Tsh. 200/=, kalamu tatu za risasi (penseli), @ tsh. 100 au

tsh. 300. rula tsh. 500/= na mkebe tsh. 2,500/=

Mahitaji hayo yote pia yanapatikana kwenye duka la shule kwa gharama zilizoainishwa

hapo juu isipokuwa Viatu na Mabegi.

NB: Waweza kuwasiliana na wauzaji katika duka la shule kwa namba za simu 0755717362 au

0755486525.

Page 5: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 5 kati ya 15

MUHIMU:

Mzazi / Mlezi unatakiwa kumnunulia mwanafunzi vitabu vifuatavyo. Pia vinapatikana

kwenye duka la shule kwa bei zifuatazo:

i. Basic mathematics book one by TIE au by Oxford. Tsh. 15,000/=

ii. Biology Book1 & 2 by Oxford. Tsh. 15,000/=

iii. Chemistry Book 1 & 2 by TIE. Tsh. 18,000/=

iv. Physics Book 1 & 2 by TIE. Tsh. 18,000/=

v. Geography Book 1 & 2 by TIE. Tsh. 18,000/=

vi. History Book One by TIE. Tsh. 15,000/=

vii. Civics Book 1 & 2 by TIE. Tsh. 18,000/=

viii. Kiswahili Kidato cha Kwanza by Oxford. Tsh. 12,000/=

ix. The Bible Revised standard version. Tsh. 15,000/=

x. Advanced learner’s Dictionary by OXFORD. Tsh. 40,000/=

xi. Kamusi Sanifu ya Kiswahili by TUKI. Tsh. 20,000/=

xii. Atlas. Tsh. 22,000/=

SEHEMU C: ANGALIZO KWA MZAZI/MLEZI

(i) Fedha yoyote itakayolipwa kwa mhasibu haitarudishwa tena kwa mteja

(ii) Shule inafuata mihula inayotolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, hivyo

itakuwa na mihula mirefu miwili na mifupi miwili kwa mwaka. Mzazi/mlezi

unaombwa kutoa ushirikiano wako kuhakikisha mtoto anawasili kwa wakati shuleni,

vinginevyo sheria itachukua mkondo wake.

(iii) Mawasiliano yoyote kati ya mwanafunzi na mzazi/mlezi yafanyike kwa kupitia Mkuu

wa shule makamu mkuu wa shule, ofisi ya Taaluma na ofisi ya Malezi. Mwanafunzi

haruhusiwi kuwa na simu ya mkononi awapo shuleni.

(iv) Shule haina utaratibu wa mzazi/mlezi kumwona mwanafunzi isipokuwa mzazi ataitwa

na uongozi wa shule kama kuna ulazima wa kufanya hivyo

(v) Mzazi/mlezi unashauriwa kutompa mtoto fedha nyingi ambazo zitamfanya apoteze

utulivu wa maisha ya shule na kuvunja sheria za shule.

(vi) Shule ina utaratibu wa kushughulikia usafiri kwa wanafunzi wanaotoka mbali kipindi

shule inapofunga. Hivyo, mzazi/mlezi utapewa taarifa kabla ya shule kufunga.

(vii) Mzazi hakikisha unapima afya ya mwanao kwa uaminifu na kutoa taarifa za kweli kwa

mwanafunzi mwenye matatizo ya kiafya kwenye uongozi wa shule na kwenye fomu

(Medical Examination Form) ili kuepuka usumbufu wakati wa masomo. Mwanafunzi

mgonjwa atapewa huduma ya kwanza katika zahanati ya shule na endapo atazidiwa

atapelekwa hospitali.

(viii) Shule haitoi chakula maalumu (special diet) kwa mwanafunzi mgonjwa.

(ix) Mzazi/mlezi huruhusiwi kumletea mwanafunzi chakula cha aina yoyote kutoka nje ya

shule.

Nakutakia Baraka za Mungu na maandalizi mema.

_ J.KAMETE

MKUU WA SHULE

Page 6: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 6 kati ya 15

SEHEMU D: MAELEZO JUU YA TAARIFA BINAFSI ZAMWANAFUNZI

(IJAZWE NA MZAZI /MLEZI NA KURUDISHWA SHULENI)

1. JINA LA MWANAFUNZI ------------------------------------------------------------------------

2. JINSIA: KE -------------------------------------------------

3. TAREHE YA KUZALIWA ----------------- MWEZI --------------- MWAKA ---------------

WILAYA ----------------------------------------- MKOA --------------------------------

NCHI ------------------------

4. NINI MALENGO YAKO YA KUSOMA? (Unataka kuja kuwa nani katika maisha yako baada

ya masomo?)………………………………………………………………………..

……………………………………………………………………………………………..

5. DINI-----------------------------------

6. KABILA ---------------------------------------------

7. URAIA -----------------------------------------------

8. JINA LA MZAZI/MLEZI -------------------------------

ANUANI ----------------------------------------

SIMU --------------------------------------------

HISTORIA YA MWANAFUNZI

1. JINA LA BABA ----------------------------------------------------

2. JINA LA MAMA -------------------------------------------------

3. JINA KAMILI LA MLEZI (AISHIYE MBEYA)

----------------------------------------------------------------------

4. KAZI YA MZAZI/MLEZI (MKULIMA/MFANYAKAZI/MFANYABIASHARA)

-------------------------------------------------

5. TATIZO LA KIAFYA ALILONALO ---------------------------------------------

6. SHULE ALIKOTOKA ---------------------------------------------

7. NAMBA YA MTIHANI______________________________

SHULE WILAYA DARASA MWAKA

Iwapo mzazi/mlezi hapatikani wafuatao utawala waweza kuwasiliana nao (ambao lazima wawe watu

wazima wanaoweza kutoa msaada na taarifa sahihi za mwanafunzi)

NA JINA UHUSIANO ANAPOISHI SIMU

1

2

3

Mimi mzazi/mlezi wa mwanafunzi mtajwa hapo juu nathibitisha taarifa hii ni sahihi.

Sahihi ya mzazi -------------------------------- Tarehe ----------------------------------------

Page 7: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 7 kati ya 15

SEHEMU E: TAMKO RASMI LA KUKUBALI NA FASI YA KUJIUNGA NA

SHULE (IJAZWE NA KURUDISHWA SHULENI)

(a) Mimi ______________________________ambaye ni mzazi/mlezi wa

mwanafunzi________________________________nimezisoma, nimezielewa na

kukubali taratibu na sharia za shule hii.

(b) Nakubali nafasi niliyopewa ya kidato cha__________ mwaka____________ kwa ajili

ya mtoto wangu.

(c) Naahidi kutekeleza yafuatayo:

i. Kulipa malipo yote kama ilivyoainishwa

ii. Kushirikiana na shule katika malezi na kufuatilia maendeleo ya taaluma ya mtoto

ili aweze kufikia kiwango kizuri cha ufaulu na nidhamu.

iii. Kumuelimisha mtoto kufuata na kutekeleza sheria na taratibu za shule kama

zilivyoainishwa katika fomu ya kujiunga.

(d) Nakubali kuwa nitashirikiana na shule katika kumsimamia mtoto wangu kitaaluma ili

aweze kufikia kiwango cha ufaulu wa zaidi ya wastani wa 60. Chini ya ufaulu huo

itabidi tushauriane.

Sahihi ya mzazi/mlezi___________________ Tarehe___________________

Page 8: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 8 kati ya 15

SEHEMU F: SHERIA ZA SHULE

1. Mwanafunzi anatakiwa kuwaheshimu walimu wote na wafanyakazi wasio walimu na mtu

yeyote aliyemzidi umri awapo shuleni na mahali pengine popote hiyo ni pamoja na

kuchuchumaa chini anaposalimia mtu yeyote aliyemzidi umri, pia ni wajibu wake

kumpokea mwalimu/mfanyakazi na mtu yeyote aliyemzidi umri anapopita/kuingia popote.

Kushindwa kufanya hivyo ADHABU KALI ITATOLEWA KWA ATAKAYEENDA

KINYUME NA SHERIA HII.

2. Ni lazima mwanafunzi aoneshe nidhamu ya kiwango cha juu katika maongezi na

wanafunzi wenzake, wazazi wake/walezi wake bila kutumia lugha ya

matusi/chafu/mitaani/kejeli/ubishi/dharau/kuzomea/kufyonza. Kushindwa kufanya hivi

kutasababisha mwanafunzi KUSIMAMISHWA MASOMO/KUFUKUZWA SHULE.

3. Mwanafunzi anatakiwa kuishi kwa amani, heshima, utii usikivu na upendo kwa watu wote,

hivyo hapaswi kupiga/ kupigana kushiriki uovu wa aina yoyote ile popote ikiwa ni kwa

kuona/kusikia, kufanya kosa lolote la jinai. Ni wajibu wake kutoficha siri ya uovu wowote

aliouona/kuusikia, kupatikana na kosa lolote katika haya kutasababisha mwanafunzi huyu

KUFUKUZWA SHULE MOJA KWA MOJA BILA MSAMAHA.

4. Mwanafunzi akikamatwa na makosa yafuatayo; wizi, ulevi, uvutaji sigara, uasherati,

kufanya mapenzi, kujihusisha na mazungumzo ya mapenzi, kusagana, kupata mimba/kutoa

mimba, kutoka au kulala nje ya shule, kuingia kwenye vilabu vya pombe/kumbi za starehe,,

kutumia madawa ya kulevya, kuandikia barua ya mapenzi, Kwa kosa lolote katika hayo

mwanafunzi ATASIMAMISHWA MASOMO/ATAFUKUZWA SHULE MOJA KWA

MOJA BILA MSAMAHA.

5. Mwanafunzi haruhusiwi kuvaa kofia, viatu vyenye kisigino kirefu, visivyo na kamba,

heleni, mikufu, kanga, bangili, pete, sketi fupi za kubana/mipasuo. Marufuku kufuga

nywele, kupaka rangi kucha au nywele, kujichubua, Yeyote atakayepatikana na haya

atarudishwa nyumbani kumleta mzazi au mlezi pamoja na ONYO KALI.

6. Mwanafunzi haruhusiwi kumiliki simu, redio, kamera, CD, DVD, pasi, hita, mshumaa,

silaha yoyote mfano kisu, chupa. Aidha, kuwa na dawa za aina yoyote bwenini, kwa kila

kosa adhabu yake ni KUFUKUZWA SHULE BILA MSAMAHA.

7. Mwanafunzi anatakiwa kuvaa sare wakati wote awapo darasani, atokapo nje ya Shule

aendapo kanisani, aingiapo shuleni, anaposafiri kuja shuleni, aendapo hospitali, kushindwa

kufanya hivyo ni kosa linalosababisha mwanafunzi KUFUKUZWA/KUSIMAMISHWA

SHULE.

8. Shule yetu ni ya Kikristo, hivyo mwanafunzi anatakiwa kufuata taratibu zetu kuhusiana na

ibada na vipindi vya dini. Kushindwa kutii ni kosa ambalo halitavumiliwa na adhabu yake

ni KUFUKUZWA SHULE.

9. Ni marufuku mwanafunzi kuletewa chakula chochote kutoka nje ya Shule kwa sababu za

kiusalama, Pia haruhusiwi kupokea na kuongea na mgeni yeyote, Mzazi au Mlezi

aliyeandikishwa na kutambulishwa na ofisi ndiye anayeweza kuonana na mwanafunzi ikiwa

ulazima utajitokeza ataruhusiwa. Aidha, Mzazi/Mlezi huruhusiwi kuonana na mwanafunzi

na hatuna siku maalumu ya kuja kumuona mwanafunzi (visiting day) kukiuka sheria hii

ADHABU KALI ITACHUKULIWA.

Page 9: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 9 kati ya 15

10. Ni lazima mwanafunzi aripoti Shule inapofunguliwa na isizidi saa nane kamili mchana.

Mwanafunzi anayechelewa hatapokelewa badala yake ATARUDISHWA NYUMBANI

KUMLETA MZAZI.

11. Ni wajibu wa mwanafunzi kushiriki kazi za mikono mf. Usafi wa mazingira, kufyeka

(kufagia), Ujenzi kilimo. Kukataa kufanya hivyo ADHABU KALI

ITATOLEWA/KUMLETA MZAZI.

12. Mwanafunzi haruhusiwi kuvaa ndala/viatu vya wazi (open shoes) popote isipokuwa

bwenini tu. Kukiuka hivyo ADHABU KALI ITACHUKULIWA.

13. Mwanafunzi anatakiwa kuheshimu Bendera ya Taifa, Nembo ya Taifa, Wimbo wa Shule,

Fedha na picha za Viongozi na alama nyingine za Taifa. Aidha, kuheshimu miito yote ya

kengele, Kutofanya hivyo ADHABU KALI ITACHUKULIWA.

14. Mwanafunzi anatakiwa kuwa safi wakati wote, kulala katika sehemu aliyopangiwa kwa

wakati unaotakiwa, kutolala wawili kitanda kimoja na kuhakikisha kuwa bweni lake na

darasa ni safi wakati wote ikiwa pamoja na sehemu ya kulia chakula na ukumbi. Kushindwa

kufanya hivyo ni kosa na ADHABU KALI ITATOLEWA.

15. Mwanafunzi haruhusiwi kufanya mawasiliano na Mzazi /Mlezi bila ruhusa ya uongozi wa

Shule, pia mwanafunzi anatakiwa kuomba, kibali maalumu endapo kutakuwa na tatizo

litakalomlazimu mwanafunzi kuhudumiwa nje ya Shule. Kutofanya hivyo kutasababisha

KUSIMAMISHWA SHULE/KUMLETA MZAZI.

16. Mwanafunzi anatakiwa kufanya bidii sana katika masomo/darasani, mwanafunzi mvivu

hatavumiliwa, endapo atashindwa kufikisha kiwango cha alama zilizowekwa na uongozi wa

Shule (wastani wa alama 50 kidato cha kwanza, cha pili, cha tatu kwenda cha nne na kwa

kidato cha tano kwenda cha sita ni lazima mwanafunzi afikishe ufaulu wa daraja la pili

(Division Two) vinginevyo ANAPASWA KUMLETA MZAZI.

17. Mwanafunzi hapaswi kupiga kelele anapokuwa katika mazingira ya Shule (yaani darasani,

bwenini, mesini) na asitoke bila ruhusa ya mwalimu au kiongozi aliyepo, Aidha,

mwanafunzi anatakiwa kuhudhuria Shule muda wote wa masomo ndani na nje ya darasa

(Ruhusa yoyote ya kutohudhuria darasani itatolewa na Mkuu wa Shule tu au mwalimu

atakayekuwa ameteuliwa na Mkuu wa Shule mfano: Makamu mkuu wa shule, Mwandamizi

taaluma, Nidhamu n.k. Kukaidi ni makosa hivyo mwanafunzi anaweza KUSIMAMISHWA

AU KUFUKUZWA SHULE.

18. Mwanafunzi anatakiwakuhudhuria na kuheshimu maandalizi ya jioni na asubuhi (Night and

Morniing preparations) Kushindwa kufanya hivyo mwanafunzi anatakiwa akamlete

Mzazi/Mlezi na ADHABU KALI ITATOLEWA.

19. Mwanafunzi mwenye matatizo ya kiafya atatakiwa aoneshe cheti cha tatizo lake mara

anapo ripoti Shule au apatapo hicho cheti cha daktari wa hospitali ya serikali au hospitali

inayotambuliwa ndicho kitakachokubalika kuoneshwa kwa Nesi wa Shule, matron au

mwalimu mwandamizi nidhamu. Kinyume na hivyo AMLETE MZAZI.

20. Mwanafunzi haruhusiwi kuandika maandishi kitabuni, katika dawati, meza, viti, au kwenye

kuta za majengo ya Shule. Kukaidi kutii hilo ni makosa hivyo mwanafunzi anaweza

KUSIMAMISHWA AU KUFUKUZWA SHULE.

Page 10: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 10 kati ya 15

21. Mawasiliano yote ya mwanafunzi awapo shuleni yatakuwa kwa lugha ya KIINGEREZA.

Hivyo ni wajibu wake kujifunza lugha hiyo kwa bidii na kuongea muda wote. Kutozingatia

hili MWANAFUNZI ATAPEWA ONYO KALI/ KUSIMAMISHWA MASOMO.

22. Matatizo au mapendekezo yawasilishwe kwa kupitia serikali ya wanafunzi au uongozi wa

Shule kukiwa na tatizo lolote kwa ufumbuzi wa mara moja, Uongozi hautavumilia

mwanafunzi yeyote atakayejihusisha na maandamano au migomo ya aina yoyote. Kufanya

kosa hilo kutasababisha mwanafunzi KUFUKUZWA SHULE MOJA KWA MOJA BILA

MSAMAHA.

23. Ni lazima mwanafunzi aamke na kulala kwa wakati na muda uliopangwa na uongozi wa

Shule, Vinginevyo mwanafunzi atarudishwa kumuita mzazi/mlezi wake na ADHABU

KALI ITATOLEWA DHIDI YAKE.

24. Ni wajibu wa mwanafunzi kulinda mali zote za Shule kama dawati na meza anayokalia,

vifaa vya usafi, kutokuharibu majengo ya shule na samani zote, vinginevyo itamlazimu

kulipia mali yoyote ya shule atakayoharibu iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya.

Kushindwa kufanya hivyo atapaswa AMLETE MZAZI PAMOJA NA FIDIA.

25. Mwanafunzi haruhusiwi kukata mti katika mazingira ya Shule, na kutunza mazingira hayo

ni wajibu wake, kuokota karatasi pale anapoziona na kutotupa karatasi ovyo. Kushindwa

kufanya hivyo kutamfanya mwanafunzi KUSIMAMISHWA MASOMO/KULIPIA MTI

ALIOUKATA.

26. Mwanafunzi anatakiwa kuhudhuria darasani muda wote wa masomo awapo shuleni hivyo

hatakiwi kuonekana bwenini wakati wa vipindi/masomo pasipo ruhusa kutoka kwa uongozi

wa Shule. Vinginevyo ATARUDISHWA NYUMBANI KUMUITA MZAZI na ADHABU

KALI ITATOLEWA.

27. Mwanafunzi haruhusiwi kudanganya katika mitihani yoyote ile iwe ya ndani au nje,

kufanya kosa hilo kutasababisha mwanafunzi KUFUKUZWA SHULE KABISA BILA

MSAMAHA.

28. Ni marufuku mwanafunzi kutembelea au kuingia nyumbani kwa mwalimu au wafanyakazi

wasio walimu bila ruhusa maalumu. Pia huruhusiwi kuingia jikoni isipokuwa kwa kibali

maalumu. Kukaidi hili HATUA KALI ZA KINIDHAMU ZITACHUKULIWA PAMOJA

NA KUMUITA MZAZI.

29. Ni kosa kwa mwanafunzi kumkimbia mwalimu au mfanyakazi yeyote, aidha kumgomea

mwalimu, Mfanyakazi asiye mwalimu au kiongozi, kosa hili litamsababishia mwanafunzi

KUSIMAMISHWA MASOMO AU KUFUKUZWA SHULE.

30. Mwanafunzi anatakiwa kuzingatia muda uliopangwa, hii ni pamoja na kuwepo eneo husika

kwa muda husika. Vinginevyo ADHABU KALI ITATOLEWA JUU YAKE.

31. Mwanafunzi haruhusiwi kuingia bwenini na chakula au sehemu nyingine yoyote isiyo

rasmi kulia chakula. Kufanya hivyo ADHABU KALI ITATOLEWA.

Page 11: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 11 kati ya 15

SEHEMU H: ANGALIZO KWA MWANAFUNZI

1. Mwanafunzi haruusiwi kupokea kitu chochote kutoka kwa mtu yeyote kutoka nje ya shule

pasipo ruhusa ya ofisi husika hii ni pamoja na kufanya mazungumzo na mgeni yeyote.

2. Mwanafunzi anatakiwa kufanya bidii katika masomo na kuhakikisha anafikisha wastani wa

60 katika mitihani yake yote.

3. Mwanafunzi haruhusiwi kuandika maandishi katika samani za shule, (meza, viti, dawati),

kuta za shule na vitabu.

4. Mwanafunzi hatakiwi kupita eneo lisilo la barabara maalumu na kutupa takataka maeneo

yasiyo rasmi au kuziona na kutoziondoa, pia haruhusiwi kukata miti katika mazingira ya

shule.

5. Mwanafunzi hatakiwi kutembea kilegevu katika eneo la ukakamavu.

6. Ni marufuku kwa mwanafunzi kutembelea sehemu zifuatazo isipokuwa kwa kibali maalum.

i) Ofisi ya walimu (staffroom)

ii) Ofisi za shule

iii) Maabara

iv) Jikoni

v) Nyumba za wafanyakazi.

NB: Kukiuka mojawapo ya kanuni na maangalizo haya kutasababisha mwanafunzi

kupewa adhabu kali.

Page 12: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 12 kati ya 15

SEHEMU I: FOMU YA UTII WA KANUNI ZA SHULE NA TABIA

NJEMA (IJAZWE NA KURUDISHWA SHULENI)

Mimi____________________________________________(jina kamili) ninatambua wajibu wangu

kama mwanafunzi na ninaahidi

(a) Sita kosa au kuchelewa kipindi chochote darasani bila ruhusa

(b) Kwamba nitatii na kuwaheshimu viongozi wangu wote kuanzia ngazi ya Kiongozi wa

darasa,Viranja wa shule,walimu,watumishi wasio walimu hadi mkuu wa shule

(c) Kwamba nimezisoma na kuzielewa na nitafuata sheria na kanuni zote za shule pamoja na

maelekezo yote yatakayotolewa mara kwa mara na uongozi wa shule.

(d) Kwamba sitatoka nje ya shule bila ruhusa ya uongozi wa shule.

(e) Kwamba kama nitashindwa kufuata hayo yote hapo juu, hatua kali ichukuliwe dhidi yangu

ambayo ni pamoja na kufukuzwa shule au kusimamishwa masomo .

Tarehe…………………… ………………………………………………….

Jina na sahihi ya mwanafunzi

Tarehe……………………. ………………………………………………

Jina na sahihi ya shahidi mzazi/mlezi

Tarehe…………………… ………………………………………………..

Sahihi ya mkuu wa shule

Page 13: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 13 kati ya 15

HHHAAARRRRRRIIISSSOOONNN UUUWWWAAATTTAAA GGGIIIRRRLLLSSS’’’ SSSEEECCCOOONNNDDDAAARRRYYY SSSCCCHHHOOOOOOLLL

Email: [email protected]

Website: www.uwata.org

“EDUCATION IS A SUSTAINABLE ASSET”

______________________________________________________________________________

MEDICAL EXAMINATION FORM

This form consists of section A to be completed by the applicant and section B to be completed

by a registered medical doctor from a recognized government hospital. The completed form

must be submitted along with other application materials.

(Please write in block letter ) .PERSONAL INFORMATION

Full name First Middle Last

Date of

birth

……../………/…….. ………LEVEL

II PAST MEDICAL HISTORY

(I)NERVOUS SYSTEM)

Any loss of consciousness ?Yes/No

If yes, date of incident_____________________

Current treatment_________________________

Any fits? Yes/No

If yes ,type of

fits__________________________

Date of last episode______________________

Current treatment_________________________

(II)MUSCULO-SKELETON SYSTEM

Any deformity? Yes/No

If yes ,which part of the body________________

Use of accessory or aids____________________

(III) OTHER CHRONIC CONDITIONS

HIV/AIDS? Yes/No

If yes ,current treatment____________________

Skin disease? Yes/No

If yes ,which type________________________

Current treatment_________________________

Allergies? Yes/No

If yes ,date of last reaction__________________

Cause of reaction_________________________

Asthma? Yes/No

If yes, when detected __________________

Current treatment____________________

Any heart disease? Yes/No

If yes what disease? ___________________

Current treatment_____________________

Major surgeries? Yes/No

If yes type of surgery__________________

Date of surgery _______________________

Any dietary restrictions? Yes/No

If yes, state restriction__________________

Any history of peptic ulcer disease?

Yes/No

If yes, current treatment________________

III.DECLARATION

I declare that all the information provide above is true to the best of my knowledge

Signature…………… Date……/…../………

SECTION A (TO BE COMPLETED BY THE APPLICANT)

Page 14: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 14 kati ya 15

SECTION B

(TO BE COMPLETED BY REGISTERED MEDICAL DOCTOR)

A.PHYSICAL EXAMINATION

1. Skin disease__________________________________________________________________

2. Eye conjunctiva Pupils

Sight: Without glasses Right _______________________________

Left _______________________________

With glasses Right ________________________________

Left________________________________

3. Please state condition of ears (if any discharge) ___________________________________

Mouth and throat _____________________________________________________________

4. Respiratory system:

Any abnormality? ______________________________________________________________

5. Cardiovascular system

Blood pressure: systolic___________________________________________________________

Diastolic_________________________________________________________

Heart: any murmur? Yes/No

If yes which type? _______________________________________________________________

6. Abdomen

Masses_________________________________________________________________

Liver _______________________________________________________________

Spleen _______________________________________________________________

Kidneys ______________________________________________________________

Any operation scars_____________________________________________________

7. Any clinical evidence of gastric /duodenal ulcer?________________________________

B. LABORATORY TEST

1. Urine pregnancy test________________________________________________________

2. Urinalysis

Albumin___________________________________________________________

Sugar_____________________________________________________________

Leukocytes _______________________________________________________

Bilharzia___________________________________________________________

3. Stool analysis____________________________________________________________

4. Blood examination: Hemoglobin__________________________________________________

White blood cell count total____________________________________

Different count:

(a) Neutrophils ___________________________________________

(b) Lymphocytes _________________________________________

(c) Monocytes____________________________________________

(d) Basophils ____________________________________________

(e) Eosinophils ___________________________________________

Page 15: H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU GGGIIRRL …harrisongirls.ac.tz/school_info/Form One (I) Joining... · 2020. 1. 10. · Ukurasa wa 1 kati ya 15 H HHA AAR RRRRI IISSSO OON NN UUU

Ukurasa wa 15 kati ya 15

I have examined Miss ______________________________________And consider that she is not/fit

to be admit to school (Delete which is not applicable)

________________________________

_________________________

DATE SIGNATURE

Authorized Medical Practitioner: Name___________________________________________

_________________________ ________________________________

Title Qualification Address________________________________ ________________________

_______________________________

________________________________ Official stamp or seal

_______________________________

SECTION C :CONCLUSION